Wednesday, February 17, 2016

MALUMBANO YA HOJA PART 1



Objet: MALUMBANO 4
Date: Dimanche 25 mai 2008, 20h36
LES ELUS
WACHAGULIWA WAKIWA IBADANI



Wachaguliwa tusikate tamaa
1.   MUNGU MKUBWA  hana choyo. Yeye amemjaalia kila mtu aliyekamilika, kuwa na uwezo na ujasiri wa kuyakabili magumu kwa uvumilivu na subira na mwishowe kuibuka akiwa mshindi.
2.   Katika kupanda, kuotesha, kupalilia na kuwekeza mbegu ya harakati ya kujiweka huru, au kuondoa bendera ya uhuru wa wachache wanaowatia utumwani walio wengi, kutokata tamaa ndiyo moyo unaosukuma damu ya mafanikio.
3.    Cha msingi ni kuweka nia pamoja na mikakati ya kujinasua bila kuzembea, iwekwe jitihada kunyanyua mguu, kukata myororo, kuvunja pingu na kupiga hatua kuelekea kwenye ngome za wakandamizaji na kuwapokonya silaha za domo na za ujuzi wote.
4.    Kunahitaji moyo Na ujasiri WA kuyaendeleza matokeo mazuri ya kutoka minyororo hadi kuwazingira waliotuweka zizini wakatufanyisha kazi kiroho na kimwili pasipo sisi kujitambua;ni hawa wanefili wenye sifa na akili za giza, watoto wa muharibifu shetani,wanao kula nyama na damu za watu,na kuwafanya wengine watumwa milele kwa njia ya elimu dunia.
5.    Leo watu wengi wamekuwa maskini saana duniani, na wanakufa kwa njaa pia magonjwa ya ovyo;ijapokuwa Muumba wa mbingu na dunia amefanya yote bora, ili mwana adam arizike na ardhi aliyowekwa aitawale.
6.    Mbona itakuwa misharabaka mikubwa,wakati maskini,watajitokesha ndani ya shimo zao za ufichoni na kuwashambulia watawala wa dunia hii kwenyi magorofa ya ustarehe wao,ili wapate maji masafi na mkate wa kula.Itakuwa mwanzo wa vita vya mwisho,duniani;kwani vita vya ARMAGIDONI ni vita vya kiroho,yaani vyaa makanisa,pia vita kati ya matajiri na wa maskini. Sela.
7.    wakimbizi wanaoweza kuswagawa na kufanikiwa kuwadhibiti wasiwepo nchini. Wapo mamilioni, wanachotakiwa ni kujipanga safi na kusonga mbele kwa namna itakayowatatiza wasifanye uharibifu wananchi pale wanapozuia sahani ya mlo isiwaondoke.
8.    Munanyanyasa wakimbizi leo na wageni ;kesho mutakuwa wakimbizi,hadi kwa inji za juu ;mbalamwezi na nyota zitawapokea na hamutaonaka dunia hii takatifu tena.Kwani katika dunia zisizo onekani zilizo nyingi kama ma elfu ;hamna hewa,mwangaza,wala udogo wa mibaraka ;kama dunia aliyopewa ADAM na HAWA.Nayo maficho ya bustani la EDENI,ni uel mji wa baraka,tokea mlima wa Abale ;muwe mukijua.
9.    Wakati wa kubariki pembe ine za dunia munaimba wimbo huu ; « WATU WA INCHI ZINGINE,WATAKUJA SHUHUDIA »Wakati wa kusonga mbele wimbo uwe, "Ninaye Mungu Mukubwa AHMIRADO,jemadari wangu,atashinda vita".
10. Lengo kila mchaguliwa aelewe kuwa kukata tamaa ni sawa na kukaza kitanzi(Kamba) shingoni. Ni sumu inayoua akili na moyo vifanye jitihada za kujing'oa kwa makucha.
11. Songa mbele tu,na songa ugali kubwa na mchuzi nzuri,ukipata ule mda na ile bahati ;sababu,wakati adui atakuja ;atakuteka nyara na utaacha chungu chako jikoni,kiliwe na umbwa.Karamu na karamu,ziwe kwako siku zote,utakapo kumbuka ukombezi wako wa tarehe 28 na tariki 3 mwezi wa 6.
12. Kiasili muhimu katika kanisa la upendo itakuwa,kunona kwa binti na wavulana wako.Usafi wa watoto na wazee wako,uzuri wa nyumba na mahali munapokaa,bonde za maua na nyimbo za kudondoza roho,pia kusisimua nywele.Sela.
13. Mchaguliwa hakutumwa kushindwa ku dunia.hata katika michezo za kandana na mitihani za shule, ao zoezi zingine ;awe kwa mustari za mbele tu.Bila hivyo ;ni aibu kubwa sana mno.
14.  Kila mtu, atafurahia utamu wa matunda ya mafundisho ya kitabu chenyi mihuri saba ;naye atauzingatia saana katika moyo wake,ili atembee kwa njia aliyo amuriwa.Ni ndani yake njoo wafalme wa dunia itakayokuja na wakubwa wengine wote,watatoke.Muwe mukijua.
15. Bendera iliyo simamishwa mbele yenu,toka mbingu ya tatu,aliyoshuka nayo,baba mtukufu ;ni bendera ya upendo.Moyo wakujitolea na damu iliyo mwangika ajili ya ukombozi wa wengine watu.Mujue kujitolea sasa.Dunia ni ya mda mfupi.
16. Wachaguliwa wana nguvu, wakiamua wanaweza kuitumia kujitia utumwani wakikata tamaa kwa kudhani kuwa ni Mungu Mkubwa ndie anayetaka wawe hivyo chini zaidi.Kumbe ni kusitasita njo inawakasesha vyote.
17. Ikidhaniwa Mungu ndiye anayewadumisha kwenye viti viongozi wa utawala usiojali wananchi itakuwa ni kumsingizia. Si Yeye anayewatia njaa, umaskini, maradhi na ujinga. Maana ameweka kanuni kuwa mwananchi hatovuna ila kile alichokitolea jasho na atayaona matunda yake.
18. Ni katika kanuni hii tunawakuta wazee wa watu weusi wameibuka na ushindi dhidi ya ukandamizaji wa watu weupe,kwa njia ya uhuru. Hata watu weupe, walikuwa na vita vyao vya maendeleo, kwakuvunja minyororo ya utawala wa kimabavu na ujinga,ili leo wajisikie wana tulia ki maisha na kiuchumi.
19. Walifanya jitihada za kuamshana mpaka wote wakatambua dhuluma waliyotendewa haikupangwa na Mungu. Wakawaambia mabwanyenye wa kikoloni kuwa mmetunyonya vya kutosha. Sasa tunataka jasho la kodi zetu lijenge na kuboresha afya za wananchi, nasi tupatiwe mlo kamili. Mapato ya utalii, madini, misitu, kilimo, uvuvi na viwanda yabadili vidungu (misonge) tunavyoishi ziwe nyumba.
20. Ile hali ya kusema 'sawa Bwana mkubwa'ndio padri’ na kuwatungia nyimbo, wanyonyaji wa kikoloni wakaikomesha.Lakini tukijitathmini tulivyonufaika wananchi tangu wazungu waliposhusha bendera na kufunga virago vyao. Uhuru ule uliopatikana kwa jasho la babu zetu umetekwa nyara na 'wenzetu' wachache.Makanisa zimedanganya saana kuliko chama cha wafanya siasa.Kwa hivyo, tutumikie kanisa moja tu ya kweli ;ni kanisa la UPENDO tu.
21. Hata huko awali, walikuwepo wasaliti waliowapiga bei wafalme na makuhani wakubwa wao,hata manabii walisalitiwa na ndugu zao wa karibu.Wachaguliwa wa sasa, Mungu Mkubwa atuhurumie,ile kikombe isitufikie,moyo mgumu ule,mpaka tumtoe mwana kondoo tena,ashindwe kufanya kazi yake. « SHANGWE KWAKO MWANA KONDOO,KWAKUTUFIKISHA SAYUNI ».
22. Kuna wananchi wasiopenda amani wanaotaka kuleta vurugu.Katika kila jambo, wanatafuta mizozo na fujo tu. Nyinyi musiwe hivyo, muegemee tu upande wa haki na kweli.musifuate sauti ya walio wengi tu,mara nyingi,inapoteza raia wapumbafu. Ni heri kuwa na mtawala mkali, kuliko kuwa na mtawala muongo.
23. Je, wanaochangia maji ya mshimu na ng'ombe ao nguruwe mtawaelezaje. Mtawaambia nini wanaopata maji ya bomba katika jiji,na mwishowe yaonekana kama maji yana vidudu na kugonjwesha watu ?. Mtawaambia nini eeh watawala, wakati chanjo zenu za kukingia maradhi,zageuka sumu kwa watoto na kuzagaa ukimwi kwa makusudi kwa maskini wa afrika na wa arabu.(hii ni ufunuo).
24. Kodi wanainchi wanayotoa, sherti ilipashwa kuwapa fursa ya kutunza kwa bure inchini na ukarabati wa njia hata za mashamba. Lakini, watawala wamemeza ndoano na kamba,na wanainchi wame jibebesha mizigo kama kobe,ili wafike kwenye heri,inakua ngoma. Mungu hana choyo. Wananchi watapata na kuonja matunda ya kile walichokifanyia jitihada. Wachaguliwa ;mufungue macho na mapua vizuri.Kuona sawa na kusikia harufu ya kibaya ao vurugo inayokuja mudunia munayo kaa ndani.Sela.




Baba mtukufu,
Mwangaza wa dunia.
Bujah 25/05/2008




KWA SWALI LOLOTE KUUSU HII WAWEZA KUTUANDIAKIA UKIBONYEZA HAPO CHINI
click here for a query

No comments:

Post a Comment